SHULE YA MSINGI YA CHIEF ZULU YA MKONDO WA KIINGEREZA YAZINDULIWA SONGEA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amezindua Shule ya Msingi Chief Zulu inayofundisha kwa lugha ya Kiingereza
Uzinduzi huo umefanyika leo Septemba 24, 2024 Mkoani Ruvuma ambapo Mhe. Rais amewataka Mawaziri wanaoshughulikia Elimu kuhakikisha walimu wenye uwezo wa kufundisha vizuri kwa kutumia lugha ya Kiingereza wanapatikana hata kutoka nje ya nchi.


