NYARAKA ZA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 TOLEO LA 2023, MITAALA ILIYOBORESHWA NA MIONGOZO MBALIMBALI
TAARIFA YA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA KIDATO CHA NNE ULIOFANYIKA NOVEMBA 2024
KUELEKEA UZINDUZI WA SERA MPYA YA ELIMU
ORODHA YA SHULE ZINAZOTOA ELIMU YA AMALI, SERIKALI NA ZISIZO ZA SERIKALI 2025
SERIKALI MKOANI MWANZA YAWAPA JUKUMU WALIMU KUTENGENEZA JAMII YA KISAYANSI
WALIMU wa masomo ya Sayansi katika Mkoa wa Mwanza, wamepewa jukumu la kuifanya jamii kuwa ya kisayansi kwa kuhakikisha kila mtu anayepita shuleni anapata maarifa yanayoongeza thamani ya maisha yake, akielewa na kutumia sayansi katika nyanja mbalimbali za maisha.

Jiunge nasi katika Safari hii ya Mabadiliko
NAIBU KATIBU MKUU - SAYANSI AWAKILISHA WIZARA KATIKA KIKAO CHA BARAZA LA VYUO VIKUU AFRIKA MASHARIKI
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel E. Mushi, amemwakilisha Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo, katika kikao cha Kamati Tendaji ya Baraza la Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki (Inter-University Council of East Africa - IUCEA)
Prof. Adolf Mkenda amekutana na viongozi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO)
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, leo tarehe 15 Januari 2025, Dodoma amekutana na viongozi wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) kwa lengo la kujadili ushirikiano kati ya Wizara na Jumuiya hiyo.
Prof. Adolf Mkenda amekutana na Waziri Simbachawene pamoja na Waziri Mchengerwa kujadili juu ya ajira za walimu
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, leo Januari 15, 2025, jijini Dodoma, amekutana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene, pamoja na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa.

Kikao hicho kimejadili juu ya ajira za walimu kwa kuzingatia matakwa ya utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023

