Mafanikio ya mhe. SSH katika uongozi kwa miaka miwili

Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa kulihutubia Bunge aliweka bayana dhamira ya serikali yake ya kufanya mapitio ya Sera ya Elimu ya mwaka 2014 na kufanya mabadiliko ya Mitaala iliyopo ili ielekezwe kwenye kutoa elimu ujuzi kulingana na mahitaji ya  soko  kitaifa, kikanda na kimataifa.

Ndani ya miaka miwili ya uongozi wa Rais Samia kumeshuhudiwa maboresho makubwa katika sekta ya elimu na utekelezaji wa kazi kulingana  azma yake ya kuhakikisha elimu inakuwa ni  kichocheo kikubwa cha  maendeleo kwa kutoa wahitimu wenye ujuzi na stadi. 

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS