NMAIST
TLSB
TEWW
UDOM
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
Tanzania Yashiriki Kongamano la Skauti Duniani Nchini Korea
Chama cha Skauti Tanzania kimetakiwa kuendelea kufuata na kuheshimu Katiba ambayo ndio Dira ya Chama hicho ili kuepusha migogoro.
Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda Jijini Dar es Salaam Julai 28, 2023 wakati akizungumza katika halfa ya kuwaaga na kuwakabidhi bendera Skauti wanaokwenda Korea kushiriki Jamboree.
Prof. Mkenda amesema kuwa mgogoro uliokuwepo awali ulikuwa mgumu na kwamba ulisababishwa na kutokufuata katiba au tafsiri tofauti za katiba hiyo, hivyo ni vema wote mkawa na uelewa sawa.
Mifumo ya Biogas kutumika Shule ya Mfano Iyumbu
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Franklin Rwezimula amewataka wasimamizi wa Ujenzi wa Mradi wa Mitambo ya Uchakataji maji taka, maabara na mitambo ya Biogas katika shule ya mfano Iyumbu kuongeza kasi ili kukamilisha kazi hizo.
Dkt. Rwezimula ametoa agizo hilo 31 Julai, 2023 wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa mifumo mbalimbali katika Shule mpya ya mfano iliyopo mkoani Dodoma, ambapo amewasisitiza Wahandisi kuongeza kasi zaidi ya ujenzi.
Mradi wa Uwezeshaji kupitia Ujuzi (ESP)
Uwezeshaji kupitia Ujuzi (ESP) ni mradi wa miaka 7 (2021-2028) unaotekelezwa na Jumuiya ya Vyuo na Taasisi za Ufundi Kanada (CICan) kwa ushirikiano wa karibu na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Tanzania (MOEST) kupitia Idara ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (DTVET). Mradi huu unafadhiliwa na Serikali ya Kanada.
Mradi wa BOOST
BOOST Primary Student Learning Program
Malengo ya Uanzishwaji wa Programu (MUP)
Malengo ya Programu ni kuboresha upatikanaji fursa sawa katika ujifunzaji bora wa Elimu ya Awali na Msingi Tanzania Bara. BOOST ni sehemu ya Mpango wa Lipa Kulingana na Matokeo katika Elimu awamu ya pili (EPforR II) na inachangia utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Sekta ya Elimu wa miaka mitano 2021/22 hadi 2025/26.
Matokeo Muhimu na Kuimarisha Mfumo:
Matokeo Muhimu

