Prof. Nombo aitaka COSTECH kuwa na Mfumo wa Kuratibu Tafiti
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameitaka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kuwa na mfumo mathubuti wa kuratibu tafiti mfumo ambao utaosomana na Taasisi nyingine za kitafiti.
Ametoa agizo hilo Julai 31, 2023 mjini Morogoro katika Kikao kazi cha kujadili usimamizi wa utafiti na maendeleo nchini ambapo amesema ili kutekeleza hilo kwa ufanisi wizara itaunda kamati ndogo shirikishi ambayo itapitia maoni ya kikao kazi na kuangalia sheria mbalimbali za taasisi zinazohusu masuala ya tafiti ili kutoa mapendekezo.

