Prof. Nombo aitaka COSTECH kuwa na Mfumo wa Kuratibu Tafiti

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameitaka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kuwa na mfumo mathubuti wa kuratibu tafiti mfumo ambao utaosomana na Taasisi nyingine za kitafiti.

Ametoa agizo hilo Julai 31, 2023 mjini Morogoro katika Kikao kazi cha kujadili usimamizi wa utafiti na maendeleo nchini ambapo amesema ili kutekeleza hilo kwa ufanisi wizara itaunda kamati ndogo shirikishi ambayo itapitia maoni ya kikao kazi na kuangalia sheria mbalimbali za taasisi zinazohusu masuala ya tafiti ili kutoa mapendekezo.

Swahili

Walimu watakiwa Kuwa Chachu ya Mabadiliko Matumizi ya TEHAMA Shuleni

Serikali imeeleza kuwa katika zama za Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji ni nyenzo muhimu itakayorahisisha utoaji wa elimu bora kwa ufanisi nchini.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uthibiti ubora wa shule kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Eprahim Simbeye kwenye Mafunzo ya TEHAMA kwa Walimu wa Shule ya awali na Msingi Tanzania Bara yanayofanyika katika Chuo cha Ualimu Tabora, mkoani Tabora.

Swahili

Walimu wa Masomo ya Ufundi Wapewa Mafunzo

Walimu wanaofundisha masomo ya ufundi nchini wanapatiwa mafunzo ili kuwaongezea mbinu za kuweza kufundisha masomo hayo kwa umahiri.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo mkoani Morogoro Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe amesema Wizara ipo kwenye mageuzi makubwa ya elimu ili iweze kutoa ujuzi hivyo mafunzo hayo ni katika kuwajengea uwezo walimu wa kuenenda na mageuzi hayo ya elimu.

Swahili

Waziri Mkenda ameutaka uongozi wa Bodi Maktaba wajikite katika ununuzi vitabu mbalimbali

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ameutaka uongozi wa Bodi ya Huduma za Maktaba kutoendelea na ujenzi wa majengo na badala yake wajikite katika ununuzi vitabu mbalimbali vya maktaba.

Prof. Mkenda ametoa agizo hilo Julai 28, 2023 Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Menejimenti na watumishi wa bodi hiyo ambapo amesema kazi ya bodi hiyo ni kuhakikisha kunakuwa na maktaba zenye vitabu vya kutosha ambavyo vitawezesha watanzania kupata maarifa.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS