WyEST Prof. Adolf Mkenda amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia kutoka Afrika Kusini Dkt. Bonginkosi Nzimande
Waziri Mkenda afanya mazungumzo na Waziri wa Elimu ya Juu kutoka Afrika Kusini
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia kutoka Afrika Kusini Dkt. Bonginkosi Nzimande juu ya ushirikiano katika Nyanja za elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia na Utafiti.
Akizungumza katika kikao hicho Dkt. Nzimande amemuomba Waziri Mkenda kukamilishwa kwa mapendekezo ya mkataba wa makubaliano kati ya Tanzania na Afrika Kusini kuhusu ushirikiano wa elimu ya Juu na Mafunzo ya Ufundi stadi.
Viongozi wa WyEST wamekutana na wajumbe wa Benki ya Dunia
Viongozi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wamekutana kwa mara ingine na kufanya majadiliano na ujumbe wa Benki ya Dunia juu ya ushirikiano katika utekelezaji wa mageuzi makubwa ya elimu nchini.
Akizungumza katika kikao hicho Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Serikali imekamilisha Rasimu ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 toleo la 2023 na maboresho ya mitaala ya elimu.
WANAFUNZI WANUFAIKA WA SAMIA SCHOLARSHIP WAISHUKURU SERIKALI KWA UFADHILI
SERIKALI IMETOA MAFUNZO KWA WALIMU WA SAYANSI NA HISABATI ILI KUWAPA MBINU BORA ZA UFUNDISHAJI
AFRIKA TUNAWEZA WAKATI NI SASA.
MINISTER FOR EDUCATION CONTRIBUTING TO THE DISCUSSION ON SCIENCE BEHIND HUMAN CAPITAL DEVELOPMENT
TANGAZO LA NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU
NGAZI YA STASHAHADA YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI KWA MWAKA WA MASOMO 2023/2024

