Prof. Adolf Mkenda amekabidhi bendera ya Tanzania kwa wanafunzi 30 wanaokwenda nchini China
Dkt. Rwezimula Awataka Wathibitu Ubora Kufanya kazi kwa Bidii
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Franklin Rwezimula leo Agosti 28, 2023 amekutana na Wathibiti Ubora wa Shule Kanda ya Dar es Salaam.
Akizungumza na Wathibiti Ubora hao Dkt. Rwezimula amewataka kufanya kazi kwa bidii na weledi katika kutimiza majukumu yao.
Naibu Katibu Mkuu huyo yupo Mkoani Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua Ujenzi wa Veta mpya zinazojengwa mkoani humo
Mkenda ameupongeza uongozi wa Shule ya Sekondari ya Uru - Kilimanjaro
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ameupongeza uongozi wa Shule ya Sekondari ya Uru kwa kuendelea kufanya vizuri katika mitihani ya Taifa.
Pongezi hizo amezitoa Agosti 26, 2024 Mkoani Kilimanjaro akizungumza katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa shule hiyo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki
Prof. Mkenda amesema kuwa kufanya vizuri kwa shule hiyo ni kutokana na jitihada za walimu na wanafunzi pamoja na ushirikiano mzuri uliopo kati ya shule na wazazi.
NATIONAL STRATEGY FOR INCLUSIVE EDUCATION2021/22-25/2026
Kukamilika kwa Awamu ya Kwanza na Kufunguliwa kwa Awamu ya pili ya Udahili wa Shahada ya kwanza kwa Kwaka wa Masomo 2023/2024
Waziri wa Elimu, Prof. Mkenda anawataka Wathibiti Ubora wa Shule nchini kutoa taarifa za changamoto.
Serikali itaendelea kufuatilia na kuhimiza ujenzi wa kampasi ya Chuo Kikuu cha Agha khan Mkoani Arusha
Serikali itaendelea kufuatilia na kuhimiza ujenzi wa kampasi ya Chuo Kikuu cha Agha Khan mkoani Arusha.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda Agosti 25, 2023 Jijini Arusha alipotembelea eneo litakalojengwa Kampasi hiyo.

