Prof. Nombo amekutana na watumishi wa Idara ya Uthibiti Ubora wa Shule

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo Leo Agosti 22, 2023 Jijini Dodoma, ameendelea na kukutana na Idara mbalimbali za Wizara ambapo  amekutana na watumishi wa Idara ya Uthibiti Ubora wa Shule ili kuweka mikakati ya pamoja ya kuimarisha kasi ya kuhudumia wadau.

Prof. Nombo  ameitaka Idara hiyo kuandika maandiko ya Miradi ambayo itawezesha Idara kutatua changamoto za rasilimali fedha na kuacha kutegemea fedha kutoka Miradi mingine.

Swahili

Prof. Mkenda Aipongeza Taasisi ya WAMA kwa kutoa fursa ya Elimu kwa watoto wanaotoka katika Mazingira Magumu

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ameipongeza Taasisi ya WAMA kwa kutoa fursa ya elimu kwa watoto wanaotoka katika mazingira magumu na yatima kupitia shule ya sekondari ya Wama Nayakama iliyopo wilayani Kibiti Mkoa wa Pwani na WAMA Sharaf iliyopo Mkoani Lindi.

Waziri Mkenda ametoa pongezi hizo alipotembelea shule ya Wama Nakaya Kibiti  kuona maendeleo ya elimu kwa shule hiyo ambapo amesema kinachofanywa na Taasisi hiyo ni kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha elimu bora inatolewa na kwa usawa.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS