Katibu Mkuu- Prof. Carolyne Nombo katika Kilele cha Wiki ya Ubunifu 2023

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof.Carolyne Nombo katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya Ubunifu kitaifa yaliyofanyika katika Kiwanja cha Jamhuri Jijini Dodoma amesema maadhimisho ya Wiki ya Ubunufu ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Awamu ya Sita katika kuongeza hamasa ya matumizi ya sayansi na teknolojia na ubunifu kama nyenzo muhimu ya kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Swahili

Waziri katika Kilele cha Wiki ya Ubunifu 2023

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema Serikali imedhamiria kuhakikisha masuala ya sayansi, teknolojia na ubunifu yanachochea kasi maendeleo ya uchumi nchini.

Prof.Mkenda ameyasema hayo leo Aprili 28, 2023 jijini Dodoma katika kilele cha Wiki ya Ubunifu kitaifa ambapo amesema sayansi, teknolojia na ubunifu zina mchango mkubwa wa kuchagiza maendeleo ya kiuchumi na kwamba nchi mbalimbali zimefanikiwa kutokana na kuwekeza kwenye eneo hilo.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS