NECTA Yakabidhi Vishkwambi 6,000

Kaimu Katibu Mkuu Wizra y Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe amekabidhi Vishkwambi 6,000 kwa Baraza la Mitihani Tanzania NECTA

Makabidhiano hayo yamefanyika julai 20, Jijini Dodoma.

Mdoe amesema huu ni mwendelezo wa utekekezaji wa mpango wa ugawaji vishkwambi kwa walimu na wakufunzi nchini ambavyo vilinunuliwa na Serikali na kutumika kwa ajili ya Sensa na hatimae vigawiwe kwa walimu, wakufunzi, Wathibiti Ubora na Maafisa Elimu.

Swahili

Canada Kuongeza Takribani Bilion 93 Kufadhili Elimu Tanzania

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ameishukuru Serikali ya Canada kutangaza kuongeza ufadhili wa Dolla za Canada milioni 50 takriban shilingi Bilioni 95 za Tanzania kwa ajili ya kufadhili miradi ya Elimu Tanzania.

Prof. Mkenda ametoa shukrani hizo Julai 20, 2023 baada ya Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa na mwenye dhamana ya Shirika la Maendeleo ya Uchumi la Pasifiki wa Canada Mhe. Harjit S. Sajjan, kutangaza ongezeko hilo.

Swahili

Uwekezaji mkubwa wafanyika katika kuboresha Vyuo vya Ualimu Nchini

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imefanya uwekezaji mkubwa kwenye Vyuo vya Ualimu nchini kwa kujenga majengo mapya, kukarabati pamoja na kuweka vifaa vya kufundishia na kujifunzia.

Akikagua utekelezaji wa Miradi ya Elimu katika Chuo cha Ualimu Kasulu na Kabanga yote ikiwa wilayani Kasulu Mkoani Kigoma Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Franklin Rwezimula amesema lengo ni kuhakikisha walimu tarajali wanapata mafunzo katika mazingira bora.

Swahili

Mkoa wa Kigoma wapongeza serikali kutenga sh Bilioni 36 Ujenzi Tawi la chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba (MUHAS)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano qa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango amewataka walimu kote nchini pamoja na kazi nzuri wanayoifanya kuendelea kufanya kazi kwa weledi na kujituma.

Makamu wa Rais ametoa agizo hilo wilayani Buhigwe Mkoani Kigoma alipokuwa akipokea madarasa 3, ofisi 2 yaliyokarabatiwa na Benki ya Biashara ya Tanzania (TCB) pamoja na ununuzi wa madawati 25, computer na photocopier.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS