WAZIRI MKENDA ASHIRIKI IBADA YA MAZISHI YA MZEE SILVIN MONGELLA JIJINI MWANZA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf F. Mkenda (Mb), leo tarehe 7 Juni, 2025, ameshiriki ibada ya mazishi ya kumuaga Marehemu Mzee Silvin Ibenge Emanuel Mongella.



Ibada hiyo imefanyika nyumbani kwa marehemu katika Kijiji cha Kabusungu, Wilaya ya Ilemela, Jijini Mwanza na kuhudhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali, wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Balozi Dkt. Emanuel Nchimbi.

Swahili

Prof. Mkenda ametembelea familia na kuweka Shada la Maua katika kaburi la aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda leo Alhamisi June 5, 2025 ametembelea familia na kuweka Shada la Maua katika kaburi la aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Hayati Mzee Cleopa David Msuya katika Kijiji cha Chomvu Usangi Wilaya ya Mwanga, Mkoani Kilimanjaro.



Katika salamu zake za pole kwa familia, Waziri Mkenda amesema kuwa Hayati Msuya alikuwa kiongozi mahiri na mzalendo kwa Taifa

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS