WATUMISHI WIZARA YA ELIMU WAPATIWA MAFUNZO JUU ÝA MAGOJWA SUGU

Published on Saturday 13 June, 2020 04:26:10

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa James Mdoe amesema afya ya mtumishi ni nguzo kubwa na muhimu ya uendeshaji wa shughuli za taasisi yeyote.

Akizungumza Jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kuwajengea uelewa watumishi wa Wizara hiyo kuhusu Virusi vya Ukimwi (VVU), Ukimwi na Magonjwa Sugu yasiyoambukizwa, Profesa Mdoe amesema watumishi wasipopewa mafunzo ya uelewa juu ya magonjwa hayo kuna uwezekano wa Taifa kupoteza nguvu kazi.

Naibu Katibu Mkuu Mdoe amesema magonjwa hayo yanaweza kupoteza maisha ya watumishi ama kusababisha utendaji kazi wa watumishi kushuka kutokana na kuugua mara kwa mara na kuwa na afya dhoofu.

“Watumishi ni muhimu katika taasisi yoyote, hivyo afya zao ni muhimu sana kwa taasisi. Katika utumishi wa umma kuna miongozo iliyotolewa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma na Utawala Bora ambayo inaelekeza namna bora ya kutoa huduma kwa watumishi,” amesema Naibu Katibu Mkuu.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Moshi Kabengwe akizungumza katika mafunzo hayo amesema Wizara imeamua kutoa mafunzo hayo ili kuwawezesha watumishi kupata uelewa na mbinu za kukabiliana na magonjwa hayo.

Read 2436 times

Contact

  • Name:    Permanent Secretary
  • Address: Government City
  • Mtumba Area - Afya Street
  •               P.O.Box 10
  •               40479 Dodoma
  • Tel:        +255 26 216 0270               
  •                +255 737 962 965
  • Email:    info@moe.go.tz
  • Zonal SQA Offices Contacts
Top