TANGAZO LA NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI KWA MWAKA WA MASOMO 2022/2023

Published on Friday 15 July, 2022 15:00:21

1. UTANGULIZI

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anatangaza nafasi za mafunzo ya Ualimu kwa ngazi ya Stashahada ya Ualimu wa Sekondari. Waombaji wa mafunzo haya ni wahitimu wa Kidato cha SITA wenye ufaulu wa Daraja la Kwanza hadi la Tatu (I-III). Wizara inakaribisha maombi ya kujiunga na mafunzo ya Ualimu katika Vyuo vya Serikali na visivyo vya Serikali kwa kuzingatia sifa zilizobainishwa katika tangazo hili.

2. SIFA ZA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU

Sifa za jumla za kujiunga na Mafunzo ya Ualimu Tarajali ngazi ya Stashahada ya Ualimu Elimu ya Sekondari ni wahitimu wa Kidato cha Sita wenye ufaulu wa Daraja la I-III kwa kiwango cha “Principal Pass” mbili (02) za masomo yanayofundishwa katika shule za sekondari Kidato cha I-IV. Aidha, kwa waombaji ambao moja ya “Principal Pass”mbili ni somo la Uchumi  “Economics”, wanaweza kuomba kozi za fani ambazo ni  Michezo (Physical Education and sports), Muziki, Sanaa za Ufundi (Fine Arts), na Sanaa za Maonesho (Theatre and Performing Arts).

3. AINA ZA MAFUNZO

Jedwali lifuatalo linaonesha aina ya mafunzo ya Ualimu, sifa za kujiunga, vyuo vinavyotoa mafunzo hayo na muda wa mafunzo

  1. MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI

 

Na.

AINA YA MAFUNZO

SIFA ZA KUJIUNGA

CHUO

MUDA WA MAFUNZO

 

 

 

 

 

1

 

 

 

 

 

Stashahada ya Ualimu Sayansi na Hisabati

Ufaulu wa Kidato cha VI kwa kiwango cha Daraja la I-III na alama zisizopungua ‘Principal Pass’ mbili katika masomo ya Sayansi, Hisabati na TEHAMA kwa kuzingatia Masomo yanayofundishwa katika shule za Sekondari. Masomo hayo ni: Basic Mathematics, Biology,Food &nutrition , Geography, Chemistry, Physics, Agriculture Science, Information and Computer Studies (ICS) na Computer Science.

Mamire TC, Monduli TC, Mandaka TC, Butimba TC, Klerruu TC, Songea TC, Tukuyu TC, Kasulu TC, Mpwapwa TC, Morogoro TC, Korogwe TC na Tabora TC

 

 

 

 

 

Miaka 2

 

2

 

 

Stashahada ya Sayansi ya Jamii, Biashara  na Lugha

Ufaulu wa Kidato cha VI kwa kiwango cha daraja la I-III na alama zisizopungua ‘Principal Pass’ mbili katika masomo ya sanaa yanayofundishwa katika shule za Sekondari Kidato cha I-IV. Masomo ya sanaa yanayofundishwa katika shule za Sekondari kidato cha I-IV ni : Kiswahili, English, History, Geography, Civics, Commerce na Book keeping.

Bunda TC, Mtwara (K) TC,

Marangu TC, Nachingwea TC, Shinyanga TC, Mandaka TC, Mpuguso TC, Dakawa TC,  Butimba TC, Tabora TC,

Morogoro TC, Tarime TC, Shinyanga TC, Bunda TC

 

 

 

 

Miaka 2

 

3

Stashahada ya Ualimu Michezo, Muziki, Sanaa za Ufundi na Sanaa za Maonesho

Ufaulu wa Kidato cha VI kwa kiwango cha Daraja la I-III na alama zisizopungua ‘Principal Pass’ mbili kama kama ilivyoainishwa hapa chini kwa kila kozi:

 

Butimba TC

 

Miaka 2

 

(a)    Sanaa za Ufundi:  masomo ya Fine Arts,  Basic Mathematics, Chemistry, History, Physics, English na Civil Engineering.

Butimba TC

 

Miaka 2

 

 (b)   Sanaa za Maonesho: masomo ya English, Literature in English, Kiswahili, Geography na History.

Butimba  TC

 

Miaka 2

 

 

(c)  Muziki: masomo ya ‘Music’ pamoja na masomo ya English, Kiswahili, Physics, Geography, History na Biology.

Butimba TC

 

Miaka 2

 

(d)  Elimu kwa Michezo: masomo ya Physical Education and sports, Languages, na Biology.

Butimba TC, Mpwapwa TC na Mtwara (K)

Miaka 2

 

B.  MAFUNZO YA UALIMU KAZINI (STASHAHADA YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI)

 

 

Na.

AINA YA MAFUNZO

SIFA ZA KUJIUNGA

CHUO

MUDA WA MAFUNZO

 
 

 

1

 

Stashahada ya Elimu Maalum (Mafunzo Kazini) Sekondari

Mwalimu kazini aliyepitia mafunzo ya Ualimu Ngazi ya Stashahada au Shahada na mwenye uzoefu wa kazi ya Ualimu usiopungua miaka 2; Aidha awe aliyefaulu masomo ya Sayansi katika mtihani wa Kidato cha Sita 

Patandi TC

Miaka 2

 
        UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
  1. Tangazo hili linawahusu wahitimu wa kidato cha sita waliohitimu kuanzia mwaka 2016 hadi mwaka 2022.
  2. Waombaji wa Mafunzo ya Ualimu katika vyuo vya Ualimu vya Serikali wanatakiwa kujisajili na kufanya maombi kielektroniki kupitia tovuti (tcm.moe.go.tz).
  3. Waombaji wa Mafunzo ya Ualimu kwa vyuo visivyo vya Serikali watume maombi yao moja kwa moja katika vyuo wanavyotaka kusoma na vyuo husika viwasilishe sifa za waombaji Baraza la Mitihani Tanzania kwa uhakiki.
  4. Waombaji wa mafunzo ya Ualimu katika Vyuo vya Serikali watachagua tahasusi hadi tatu (03) kwa kuanza na ile ambayo mwombaji anaipenda zaidi.
  5. Waombaji wa nafasi za mafunzo walio kazini wanaoomba kozi ya Elimu Maalumu wanapaswa kuwa wamehitimu mafunzo ya Ualimu ngazi ya Stashahada au Shahada. Aidha, waombaji walio kazini watapaswa kuambatisha barua ya kuwekwa kwenye mpango wa ruhusa ya masomo kutoka kwa waajiri wao.
  6. Majibu kwa watakaochaguliwa kujiunga na Mafunzo ya Ualimu yatatolewa kupitia “account” aliyotumia mwombaji kuomba mafunzo ya Ualimu (kuanzia 20/08/2022) na katika Vyuo vya Ualimu walivyochaguliwa.
  7. Barua na fomu za kujiunga na Mafunzo zitatolewa kupitia tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (moe.go.tz) na Chuo atakachopangwa mwombaji kwa kutumia anuani yake. Waombaji wote wanashauriwa kuandika anuani kamili, barua pepe na namba ya simu inayopatikana kwa mawasiliano zaidi.
  8. Mwisho wa kutuma maombi kwa Mafunzo ya Ualimu ni tarehe 15/08/2022.  

          Tanbihi: Masomo ya Dini hayatatumika kama kigezo cha sifa ya kujiunga na Mafunzo ya Ualimu.

Read 14334 times

Contact

  • Name:    Permanent Secretary
  • Address: Government City
  • Mtumba Area - Afya Street
  •               P.O.Box 10
  •               40479 Dodoma
  • Tel:        +255 26 216 0270               
  •                +255 737 962 965
  • Email:    info@moe.go.tz
  • Zonal SQA Offices Contacts
Top