MAPOKEZI YA VIONGOZI WATEULE, KATIBU MKUU NA NAIBU KATIBU MKUU (ELIMU)

Published on Tuesday 28 February, 2023 12:19:21

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Carolyne Nombo amewataka watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa umahiri, weledi na ubunifu ili malengo ya sekta ya elimu, Sayansi na Teknolojia yaweze kufikiwa.

Prof. Nombo ametoa wito huo jijini Dodoma wakati wa mapokezi yake na Naibu Katibu  Mkuu Dkt Franklin Rwezimula baada ya kuteuliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu, Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo amesema Wizara hiyo imepewa majukumu makubwa ya kuhakikisha elimu inayotolewa kwa watanznia inakuwa bora na kuimarisha Sekta ya Sayansi na Teknolojia.

Ameongeza hivi sasa  wizara ipo katika hatua za mwisho za kuhuisha sera ya elimu na mafunzo ta 2014 na Mitaala,huku akisisitiza kuwa si Tanzania pekee inayofanya mageuzi hayo bali Dunia nzima ipo katika kufanya mageuzi ya elimu.

"Mageuzi katika utendaji wa kufanya kazi kwa weledi,  umahiri ,  ubunifu na kwa uwazi  ni muhimu ili kufikia yale mageuzi tunayoyatamani katika sekta ya elimu", amesisitiza Katibu Mkuu.

 Prof. Nombo amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwaamini na kumpa nafasi katika utumishi huo.

Aidha amewashukuru Makatibu Wakuu waliotangulia kwa kuweka misingi imara katika kuelekea mageuzi nchini.

Naye Naibu Katibu Dkt. Franklin Rwezimula amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumuani na kumpa nafasi ya kutumikia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, huku akiahidi ushirikiano kutoka kwa watumishi ili kuendelea kuboresha sekta ya elimu.

Read 491 times

Contact

  • Name:    Permanent Secretary
  • Address: Government City
  • Mtumba Area - Afya Street
  •               P.O.Box 10
  •               40479 Dodoma
  • Tel:        +255 26 216 0270               
  •                +255 737 962 965
  • Email:    info@moe.go.tz
  • Zonal SQA Offices Contacts
Top
Kituo cha Huduma kwa Mteja