KATIBU MKUU MICHEL ATAKA WATUMISHI TET KUENDELEA KUFANYA KAZI KWA NIDHAMU, WELEDI

Published on Monday 11 July, 2022 07:38:15

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt.Francis Michael amewataka watumishi wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kufanya kazi kwa weledi, nidhamu katika kuhakikisha suala la elimu linaendelea kuimarika nchini.

Dkt.Michael ameyasema hayo leo tarehe 11/7/2022  jijini Dar es salaam alipofanya ziara katika Taasisi hiyo  ambapo amesema Serikali  inawategemea katika kusaidia utoaji wa elimu nchini.

"Nawaomba mfanye kazi kwa weledi na kuhakikisha suala la elimu na haswa haya maboresho ya mitaala yanayoendelea yafanyike vizuri,"amesema Dkt.Michael.

Aidha  Dkt.Michael amemshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kwa namna anavyoendelea kuwajali watumishi wa umma kwa kujali maslahi yao na kuwataka watumishi wa TET kutomwangusha  Rais, na badala yake wafanye kazi ipasavyo. 


Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amesema kuwa wameshukuru ujio wa Katibu Mkuu na kuwa TET inaendelea kufanya kazi zake katika kuzingatia misingi ya kiutumishi na kuwa suala la maboresho ya mitaala linaloendelea litafanyika vizuri. 

Katibu  Mkuu katika ziara yake aliambatana na Mkurugenzi wa Rasilimali watu  na Utawala wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Moshi Kabengwe.

Read 748 times

Contact

  • Name:    Permanent Secretary
  • Address: Government City
  • Mtumba Area - Afya Street
  •               P.O.Box 10
  •               40479 Dodoma
  • Tel:        +255 26 216 0270               
  •                +255 737 962 965
  • Email:    info@moe.go.tz
  • Zonal SQA Offices Contacts
Top