TUZO UANDISHI BUNIFU 13. APRILI 2023

Published on Saturday 25 March, 2023 12:44:10

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda na Katibu Mkuu Prof Carolyne Nombo leo Machi 23, 2023 wamekutana na Kamati ya Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu kwa lengo la kujadili maandalizi ya utoaji wa tuzo hizo

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika jijini Dodoma Prof Mkenda ameipongeza kamati hiyo kwa kazi kubwa waliofanya.

Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo Dkt. Salma Omar Hamad ameeleza kuwa maandalizi ya utoaji tuzo hizo yanaendelea na kwamba hafla ya utoaji tuzo hizo itakuwa Aprili 13, 2023 

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeanzisha mashindano ya Uandishi Bunifu ili kutambua na kutoa chachu kwa watanzania kuandika .  

Mashindano hayo kwa mwaka 2023 yalizinduliwa Septemba 12, 2022 .

Read 727 times

Contact

  • Name:    Permanent Secretary
  • Address: Government City
  • Mtumba Area - Afya Street
  •               P.O.Box 10
  •               40479 Dodoma
  • Tel:        +255 26 216 0270               
  •                +255 737 962 965
  • Email:    info@moe.go.tz
  • Zonal SQA Offices Contacts
Top