SERIKALI YA TANZANIA NA UINGEREZA ZA TARAJIA KUSHIRIKIANA KATIKA MRADI WA SHULE BORA

Published on Thursday 13 May, 2021 00:03:57

Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Uingereza inatarajia kutekeleza Mradi wa Shule Bora wenye lengo la kuboresha mazingira ya shule na kutoa mafunzo kwa walimu.

Hayo yamesemwa Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri anayeshughulikia masuala ya Afrika katika Serikali ya Uingereza, James Duddridge ambao pia wametembelea shule ya Sekondari Kibasila.

Waziri Ndalichako ameongeza kuwa Serikali ya Uingereza ni moja kati ya wadau muhimu katika sekta ya elimu ambapo pamoja na mambo mengine imewezesha utekelezaji wa Mradi wa Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R) na Mradi wa Kuboresha Elimu (Equip T) ambao umetekelezwa katika Mikoa tisa.

Read 2439 times

Contact

  • Name:    Permanent Secretary
  • Address: Government City
  • Mtumba Area - Afya Street
  •               P.O.Box 10
  •               40479 Dodoma
  • Tel:        +255 26 216 0270               
  •                +255 737 962 965
  • Email:    info@moe.go.tz
  • Zonal SQA Offices Contacts
Top