JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
nembo

Simu: 2121600
Fax: 022-2113271 Elimu Tz

 

KUONGEZWA KWA MUDA  WA MAOMBI YA MAFUNZO YA MUDA MFUPI YA UALIMU KWA WATAKAOKWENDA KUFUNDISHA SHULE ZA SEKONDARI
MACHI HADI APRILI 2007

Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi anatangaza nafasi 6,000 za mafunzo maalumu ya ualimu ya muda mfupi (Wiki Nne) kwa wahitimu wa kidato cha SITA wenye ufaulu wa kiwango cha “principal pass” mbili kwenye masomo yanayofundishwa katika shule za sekondari. Maombi yanawahusu pia waombaji waliosomea kozi za ufundi (Full Technician Course-FTC) na Elimu ya Biashara (Business Education). Aidha, mwombaji awe ameshinda kidato cha sita, aoneshe jinsi (Ke/Me) pamoja  na umri wake. Mafunzo yataendeshwa kuanzia tarehe 12/03/2007 hadi 07/04/2007. Maombi ya kujiunga na mafunzo yatumwe katika vyuo vya ualimu kwa kuzingatia mkoa anakotoka mwombaji kama ifuatavyo:

Chuo

Mikoa

Idadi ya nafasi

Chuo cha Ualimu Morogoro,
 S.L.B.  691, Morogoro
e-mail: ngonyaniwa@yahoo.co.uk
Simu: 0754 288766

Dar es Salaam
Morogoro

850

Chuo cha Ualimu Mpwapwa,
S.L.B. 34, Mpwapwa
e-mail: mpwatc@do.ucc.co.tz
Simu: 0784462814

Singida
Dodoma

800

Chuo cha Ualimu Tabora,
S.L.B.320, Tabora
e-mail: taboratc@taboraonline.com
Simu: 0754 979109

Tabora
Kigoma

400

Chuo cha Ualimu Tukuyu,
S.L.B. 554, Tukuyu
e-mail:tukuyutc@alma.co.tz
Simu:0754 080907

Mbeya
Rukwa

550

Chuo cha Ualimu Butimba,
S.L.B. 1411, Mwanza
e-mail:luimsoffe@yahoo.com
Simu:0754 275584

Mwanza
Shinyanga

850

Chuo cha Ualimu Kleruu,
 S.L.B.549 Iringa
e-mail:Klerruutc@iringanet.co.uk
Simu:0784 433364

Iringa

300

Chuo cha Ualimu Monduli,
S.L.B.5, Monduli
e-mail:dvdmarandu@yahoo.co.uk
Simu:0754 319504

Arusha
Manyara

550

Chuo cha Ualimu Bunda,
S.L.B. 1 Bunda
e-mail:bundatc@hotmail.com
Simu:0282621028

Kagera
Mara

450

Chuo cha Ualimu Korogwe,.
S.L.B. 533, Korogwe
e-mail:kortc@habari.co.tz
Simu:0784678136

Tanga
Kilimanjaro
Pwani

850

Chuo cha Ualimu Mtwara(K),
 S.L.B. 506, Mtwara
e-mail:mtwara@tctanzania.com
Simu:0784383151

Ruvuma
Lindi
Mtwara

400

 

          A:      MAELEKEZO MUHIMU KWA WAOMBAJI

  1. Maombi yaambatane na nakala za vyeti vya kuhitimu Kidato cha IV na cha VI pamoja na picha mbili (passport size).
  2. Maombi yaoneshe bayana masomo mawili ya CHAGUO mwombaji atakayopendelea kufundisha. 
  3. Majibu kwa watakaoteuliwa yatatolewa tarehe 05/03/2007 kupitia ofisi za maafisaelimu wa mikoa.
  4. Waombaji watakaochaguliwa watatakiwa kuonesha vyeti halisi vya kidato cha IV na cha VI wakati wa usajili.
  5. Waombaji wawe wamemaliza kidato cha sita kati ya mwaka 1998 hadi 2006.

          B:      GHARAMA ZA MAFUNZO:
Watakaochaguliwa kujiunga na mafunzo watajigharimia nauli kwenda chuoni na watarejeshewa nauli hiyo pamoja na nauli ya kwenda kwenye wilaya watakazopangiwa kufundisha. Serikali itagharimia ada ya mafunzo, vifaa vya mafunzo na chakula kwa muda wote wa mafunzo. Aidha, Mwanafunzi atajigharimia vifaa vya usafi na malazi (shuka, mto), vyombo vya kulia chakula na fedha za matumizi binafsi.

          C:      AJIRA BAADA YA MAFUNZO
Wahitimu wa Mafunzo haya maalumu ya Ualimu watapatiwa leseni ya kufundisha kwa miaka minne (4) na wtaajiriwa katika shule za sekondari za Serikali.

 

Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 28/02/2007. Unaweza pia kusoma tangazo hili katika tovuti ya Wizara: www.moe.go.tz

Hamisi O. Dihenga
KATIBU MKUU
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
S.L.P.9121, DAR ES SALAAM