JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
nembo

Simu: 2121600
Fax: 022-2113271 Elimu Tz

NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI NA STASHAHADA: JULAI 2007/2008

Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi anatangaza nafasi za mafunzo ya ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada kama ifuatavyo:

A: MAELEKEZO MUHIMU KWA WAOMBAJI

  1. Waombaji wa Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti (IIIA) watachaguliwa kupitia “Selforms”. Watakaohusika ni wahitimu wa kidato cha IV 2006 wenye ufaulu usiopungua Divisheni III.
  2. Waombaji wa Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Stashahada wawe wamehitimu kidato cha VI kati ya mwaka 1998 na 2007 na wawe na ufaulu usiopungua ‘Principal Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja.
  3. Muda wa mafunzo ni miaka miwili na mafunzo yataanza Julai 2007.
  4. Maombi yaambatane na nakala za vyeti vya Kidato cha IV, Kidato cha VI na Cheti cha Ualimu kwa wale ambao ni walimu.  Aidha maombi yaambatane na picha mbili za mwombaji (passport size).
  5. Maombi yaoneshe kiwango cha taaluma, ufaulu wa kila somo katika mtihani wa mwisho na umri wa mwombaji.  Aidha mwombaji aoneshe ni mwanamme / mwanamke na umri kazini kwa wale walioajiriwa.
  6. Upo uwezekano wa kupata mafunzo ya ualimu mwanafunzi akiwa anaishi nje ya chuo.  Endapo mwombaji atapenda kusoma akiwa nje ya chuo aeleze na ataje chuo anachopendelea kusoma.
  7. Barua za waombaji wa Mafunzo ya Walimu Kazini zipitishwe kwa waajiri.

 

B: KUAJIRIWA BAADA YA MAFUNZO

  1. Wahitimu wa Mafunzo ya Ualimu (tarajali) ngazi ya Cheti na Stashahada wana nafasi ya kuajiriwa serikalini au shule zisizo za serikali.
  2. Wahitimu wa Mafunzo ya Ualimu (Kazini) ngazi ya Stashahada Elimu Maalum, Sayansi Kimu, Sanaa Ufundi, Maonesho, Muziki na Michezo ambao wana ajira watarudi kwa waajiri wao kufundisha fani walizosomea.

C: GHARAMA ZA MAFUNZO:  Ada kwa Mafunzo ya Ualimu (tarajali) ngazi ya Cheti (IIIA) na Stashahada kwa kila mwaka wa masomo ni shs. 150,000/=.

D: Aina ya mafunzo yatakayotolewa na sifa zinazotakiwa ni kama ifuatavyo:


NA

MAFUNZO

SIFA ZA WAOMBAJI

1.

STASHAHADA YA UALIMU (TARAJALI): MUDA WA MIAKA 2

Awe amefaulu kidato cha VI kwa kiwango kisichopungua ‘Principal Pass’ moja na ‘subsidiary’ moja   katika masomo yanayofundishwa shule za sekondari.  AU awe na cheti cha FTC katika masomo ya Sayansi na Hisabati.

2.

STASHAHADA YA UALIMU (KAZINI): MUDA WA MIAKA 2

  1. Awe mwalimu anayefundisha na mwenye Cheti cha Ualimu (IIIA) na uzoefu kazini usiopungua miaka mitatu.
  2. Awe amefaulu kidato cha sita kwa kiwango kisichopungua ‘Principal Pass’ moja na ‘subsidiary’ moja katika masomo yanayofundishwa shule za sekondari.

3.

STASHAHADA YA UALIMU (ELIMU MAALUM): MUDA WA MIAKA 2

(a) Awe mwalimu mwenye Cheti cha Ualimu(IIIA) cha Elimu Maalum, na ambaye amefaulu masomo mawili Kidato cha Sita.  AU
(b) Awe mwalimu mwenye Stashahada ya Ualimu fani ya Sayansi/Sayansi ya Jamii na awe na uzoefu kazini usiopungua miaka 3.  Aina ya mafunzo:  (i) Wasioona (ii) Viziwi (iii) Watoto wenye ulemavu wa akili.
(c) Awe ameshinda Kidato cha VI kwa kiwango cha ‘Principal Pass’ moja na ‘subsidiary’ moja na anapenda kufundisha watoto wenye mahitaji maalum (wasioona, viziwi, watoto wenye ulemavu wa akili).

4.

STASHAHADA YA UALIMU SAYANSI KIMU: MUDA WA MIAKA 2

(a) Awe mwalimu mwenye Cheti cha: Ualimu Daraja IIIA, Sayansi Kimu na awe ameshinda kwa kiwango kisichopungua “Principal Pass” moja na “Subsidiary” katika masomo ya: Baiyolojia, Kemia na Sayansi Kimu katika mitihani ya Kidato cha VI.  AU
(b) Awe ameshinda kwa kiwango cha “Principal Pass” moja na “Subsidiary” katika mitihani kidato cha VI katika masomo ya Sayansi Kimu na somo mojawapo kati ya: Baiyolojia, Kemia, Kilimo, Fizikia,  Hisabati, ‘Textile’ na ‘Nutrition’.

5.

MAFUNZO YA STASHAHADA YA UALIMU (MICHEZO, MUZIKI, SANAA MAONESHO/UFUNDI). MUDA WA KOZI: MIAKA 2.

      1. Awe mwalimu mwenye cheti cha Ualimu Daraja IIIA na aliyejiendeleza hadi kidato cha sita na kufaulu kwa kiwango cha ‘’Principal Pass’’ moja na “Subsidiary”.  Kozi ya Sanaa za maonyesho, afaulu katika masomo yanayostahili: English literature, Kiswahili, Jiografia na Historia.  Kozi ya Muziki, afaulu katika masomo yanayostahili: English, Kiswahili, Muziki, Historia, Jiografia na Fizikia.  Kozi ya Sanaa Ufundi, afaulu katika masomo yanayostahili: Fine Art na /au masomo mengine.  Kozi ya Elimu kwa Michezo, afaulu katika masomo yanayostahili: Baiyolojia, Kemia, Fizikia, English na Kiswahili.

AU

      1. Awe ameshinda Kidato cha VI kwa kiwango cha “Principal Pass” moja na “Subsidiary” katika masomo yaliyotajwa hapo juu na kuonyesha uwezo, stadi, na mwelekeo katika fani anayoomba.

  (c) Waombaji wote watakaochaguliwa watafanyiwa usaili kabla ya kujiunga na mafunzo.

6.

MAFUNZO YA CHETI CHA UALIMU (SAYANSI KIMU): MUDA WA MWAKA 1

(a) Awe mwalimu mwenye Cheti cha Ualimu Daraja IIIA.
  (b)Awe na uzoefu  kazini usiopungua miaka 3.
(c ) Awe amefaulu katika mtihani wa kidato cha IV masomo ya Sayansi Kimu au Masomo ya Sayansi.

7.

MAFUNZO YA CHETI CHA UALIMU (ELIMU MAALUM): MUDA WA MWAKA 1

(a) Awe mwalimu mwenye cheti cha ualimu daraja la IIIA.
(b) Awe amefundisha kwa muda usiopungua miaka 3.
(c) Awe amefaulu masomo ya Sayansi katika mitihani ya kidato cha nne.
(d) Awe mwalimu anayefundisha Elimu Maalum bila mafunzo rasmi.

8.

DIPLOMA (Technical Education.)

Awe amefaulu na kupata cheti cha FTC kutoka vyuo vya Ufundi Arusha, Mbeya, Dar es Salaam au sifa inayolingana.

9.

DIPLOMA (Agriculture Education)

Awe amefaulu kidato cha VI kiwango cha angalau “Principal Pass” moja na “Subsidiary” katika masomo ya Baiyologia na Kilimo au sifa inayolingana.

10.

DIPLOMA (Commerce/Accauntancy)

Awe amefaulu kidato cha VI, kiwango kisichopungua “Principal Pass” moja na “Siubsidiary’” katika masomo ya Biashara na Uhasibu (Accountacy)

11.

CHETI NA MAFUNZO MAALUM YA MUDA MFUPI (LESENI YA KUFUNDISHA SHULE ZA SEKONDARI)

Awe amefaulu kidato cha VI kwa kiwango kisichopungua “Principal Pass” moja na ‘Subsidiary’ moja.  Kipaumbele ni kwa masomo ya Hisabati, Sayansi na Kiingereza.

E. Angalizo; Waombaji wenye ufaulu chini ya Principal Pass mbili watapaswa kurudia mitihani ya Kidato cha Sita wakiwa mwaka wa kwanza chuoni ili waweze kuendelea na mwaka wa pili. Aidha, waombaji wa masomo ya Sayansi, Hisabati na Lugha watapewa kipaumbele.

F:       Maombi yote yatumwe kwa kutumia anuani ifuatayo:

 

KATIBU MKUU,
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI,
S.L.P. 9121,
DAR ES SALAAM (Aione Mkurugenzi, Elimu ya Ualimu).

 

MAJIBU YATATOLEWA KWA WATAKAOTEULIWA TU.

 MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI NI TAREHE 25/05/2007.