| ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI MWAKA WA MASOMO 2012/2013 | | Print | |
|
ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI MWAKA WA MASOMO 2012/2013 MAELEKEZO MUHIMU Waombaji waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya ualimu katika mwaka wa masomo 2012/13 wanatakiwa kuripoti katika vyuo walivyopangiwa tarehe 12/08/2012. Kwa wale watakaochelewa kupata barua za maelekezo (Joining instruction) kutoka vyuoni wanatakiwa waripoti vyuoni katika tarehe iliyopangwa bila kukosa. Wanafunzi wanatakiwa kufika vyuoni wakiwa na mahitaji yafuatayo: 1.Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania Kidato cha NNE na SITA kulingana na kozi husika. 2. Ada kwa mwaka ni shilingi 200,000/=. (Muhula wa kwanza shilingi 100,000/= na muhula wa pili shilingi 100,000/=). 3.Sare ya Chuo kulingana na maelekezo ya chuo husika . 4. Fedha za matumizi binafsi. Aidha, kila Mkuu wa Chuo anatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanaosajiliwa chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na SI vinginevyo |